JB ATANGAZA KUACHANA NA KAZI YA UIGIZAJI


Msanii wa Bongo Movies, Jacob Steven maarufu kama JB ametangaza kuachana na kazi ya uigizaji na kujikita zaidi katika uongozaji na uandaaji wa filamu.

JB ameandika kupitia akaunti yake ya Instagram;- ‘’Niliwahi kusema napumzika kufanya filamu na nitabaki kwenye tamthilia.. lakini sasa Nafikiria kupumzika pia kuigiza na nitabakia nyuma ya camera kama Producer na Director.

Tamthilia yangu ya #mwanamuzikiseries nafikiri itakuwa ndio ya mwisho..kuigiza.. Ni matumaini yangu kwenye kipindi chote. Tangu 1997 wakati naanza mambo hayo mpaka 2000 wakati naanzisha Jerusalem films umefurahia kazi zangu..lakini nakuahidi huo ni mwanzo tu..mengi mazuri yanakuja nikiwa nyuma ya camera.’’

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments