NANHRI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI , TAASISI KULINDA HAKI ZA RAIA


Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Mohamedh Hamad

Na Magrethy Katengu - Dar es salaam
Mtandao wa Taasisi za Haki za Binadamu wa nchi za Afrika (NANHRI) umesema utahakikisha wanashirikiana na serikali na taasisi za kibinadamu ili haki za raia zinakuwa mtambuka ili kuchochea maendeleo ya uchumi wa nchi zote.

Akizungumza Dar es salaam mkurugenzi mwendeshaji wa mtandao wa haki za binadamu barani Afrika Gilbert Sebihogo wakati wa ufunguzi wa semina ya wadau kutoka taasisi za kiserikali na binafsi ambapo amesema semina imeandaliwa kwa lengo kuwajengea uwezo wa namna ya kusaidia raia kufahamu haki zao na kuzilinda.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini Mohamedh Hamad amesema suala la haki za binadamu ni la watu wote na serikali ina jukumu kubwa na ni lazima ishirikishe wadau mbalimbali ili haki na ulinzi wa raia ilindwe.


"Pamoja na serikali imekuwa ikihakikisha katika masuala yote yanayohusu sheria au katika wanashirikiana na Mtandao wa watetezi wa haki za kibinadamu na asasi za kiraia kutoa maoni yao kabla sheria au sera haijapitishwa na kusainiwa na Rais", alisema Mohamed.

Kwa upande Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadmu (THRDC) amesema kuna masuala ya kisheria yanahitaji wadau kutoka serikalini kwakuwa ndiyo wanaotunga sheria na mipango ya kitaifa hivyo ni muhimu wawe na mashirikiano ya pamoja ma Azaki katika suala la ulinzi wa haki za raia.

Aidha amesema kila taasisi na Watendaji wake wakifuata misingi ya sheria,kanuni na Utawala Bora misingi ya haki za Binadamu haitaweza kuvunjwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments