MFANYABIASHARA MAARUFU WA MADINI YA TANZANITE NA MMILIKI WA GOLD CREST HOTEL AFARIKI DUNIA


Mfanyabiashara maarufu wa madini ya Tanzanite, Mathias Manga aliyekuwa anamiliki mgodi wa Tanzanite wa Manga Gems uliopo kitalu D amefariki dunia leo Alhamisi Agosti 12,2021 akiendelea kupatiwa matibabu nchini Afrika Kusini.

Manga pia alikuwa Mmiliki wa Hoteli za Gold Crest zilizopo jijini Arusha na Mwanza na alikuwa anamiliki majumba kadhaa ya kifahari jijini Arusha na amewahi kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC).

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyabiashara wa Madini Tanzania (Tamida), Sammy Mollel amesema amepata taarifa za msiba wa Manga.

R.I.P Mathias Manga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments