SIMBA BINGWA VPL MARA NNE MFULULIZO



Mabao mawili ya John Bocco na Chriss Mugalu kwenye mchezo wa Ligi dhidi ya Coastal Union uliopigwa kwenye Dimba la Benjamin Mkapa yametosha kuifanya Simba kutangaza ubingwa baada ya kufikisha alama 79 ambazo hakuna timu yeyote ya ligi inaweza kuzifikisha kwa msimu huu.

Simba wamechukua ubingwa huo kwa mara ya nne mfululizo tangu walivyofanya hivyo msimu wa 2017/2018.Simba imekuwa bingwa baada ya kufikisha alama 79 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote, huku bado ikiwa na michezo miwili kibindoni ligi kumalizika.

Mbali na ubingwa, Nahodha wa Simba, John Bocco ndiye anaongoza kwa ufungaji magoli akiwa na magoli 15 hadi sasa akifuatiwa Prince Dube wa Azam FC mwenye magoli 14.

Mwamba wa Lusaka, Clatous Chama yeye anaongoza kwa assists ambapo amehusika kwenye magoli 15.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments