MHASIBU WA CHAMA CHA WAIGIZAJI TANZANIA AUA KISHA KUJIUA KWA RISASI BAA


Alex Korosso kwa jina maarufu la Simba anayedaiwa kuua na kisha kujiua, alikuwa mhasibu wa Chama cha Waigizaji Tanzania (TDFAA),imeelezwa.

Hayo yamesemwa leo Jumapili Julai 18, 2021 na mwenyekiti wa chama hicho,Chiki Mchoma maarufu kwa jina la Chiki katika mahojiano yake na Mwananchi.

Tukio la Korosso kujiua lilitokea jana baa ya Lemax maeneo ya Sinza jijini Dar es Salaam, baada ya kuibuka mabishano kati yake na mtu aliyetambulika kwa jina la Gift ambaye alimpiga risasi na kisha naye kujipiga na kufariki hapohapo.

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments