RAIS SAMIA AMTEUA BALOZI BATILDA KUWA MKUU MKOA WA TABORA, ZUWENA JIRI RAS MPYA SHINYANGA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo Ijumaa Juni 11,2021 amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Mikoa na kuteua wengine. Katika mabadiliko hayo , amemteua Bi. Batilda Salha Buriani kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora kuchukua nafasi  ya Ally Hapi ambaye anahamia mkoa wa Mara  huku aliyekuwa Katibu Tawala wilaya ya Simanjiro, Zuwena Omari Jiri akiteuliwa kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Shinyanga.

Mkuu wa Mkoa wa Mara , Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi anahamia Mkoa wa Mwanza ambapo aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Albert Chalamila uteuzi wake umetenguliwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments