ASKARI POLISI AMUUA KWA KUMPIGA RISASI JAMAA WAKIGOMBANIA MWANAMKE

Maafisa wa polisi kaunti ya Nairobi nchini Kenya wanachunguza kisa kimoja ambapo afisa wa polisi anadaiwa kumuua jamaa wa umri wa makamo kwa kumpiga risasi baada ya wawili hao kugombana kuhusu mwanamke.

Afisa huyo Titus Kipchirchiri Kirui anasemekana kumpiga risasi Charles Karugu Kikuyu mwenye umri wa miaka 32 kwa madai kwamba alikuwa akimnyemelea mpenzi wake.

 Kulingana na ripoti ya polisi, Maafisa wenzake wa polisi kutoka Embakasi waliofika katika eneo la tukio waliupata mwili wa Kikuyu ukielea kwenye damu sakafuni katika buchari moja mtaani Embakasi. 

Kikuyu alikimbizwa katika hospitali ya Mama Lucy lakini alifariki dunia kabla ya kuhudumiwa, upasuaji wa maiti unatarajiwa kufanywa wakati wowote. Kirui alikamatwa baadaye na yuko kizuizini huku uchunguzi zaidi ukiendelea. 

Maafisa wa polisi walipata risasi moja ambayo itatumika kama ushahidi katika kesi dhidi ya Kirui. 

 Chanzo - Tuko news


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments