SHINDANO LA MISS KAHAMA KUFANYIKA JUMAMOSI HII JUNI 5

Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Anamringi Macha (wa tano kulia)  akiwa na mwaandaaji wa Mashindano ya Miss Kahama, Peter  Frank Alex pamoja na baadhi ya washiriki wa shindano la Miss Kahama 2021
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Shindano la Urembo kutafuta mlimbwende wa Kahama ‘Miss Kahama 2021’ yanatarajia kufanyika Jumamosi hii June 5,2021 katika ukumbi wa African Lounge Mjini Kahama yakishirikisha warembo 12 huku Msanii Mr. Blue akinogesha mashindano hayo.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Br.Black Social Partners ambao ni waandaaji wa Shindano la Urembo la Miss Kahama, Peter Frank Alex amesema maandalizi ya shindano hilo yamekamilika.

Amesema shindano la Miss Kahama litafanyika Jumamosi hii June 5, 2021 African Lounge. Washiriki wapo 12 ambao ni mabinti warembo kutoka Kahama ambao sasa wapo kambini wanaendelea na mazoezi.

“Maandalizi ya shindano la Miss Kahama ni makubwa hivyo wananchi wategemee mambo makubwa siku hiyo kuanzia saa moja usiku. Tiketi zinaendelea kutolewa maeneo mbalimbali ikiwemo Huheso FM kwa Zakazi, BSL College, African Lounge na tunasambaza mtaa kwa mtaa na siku ya shindano tiketi zitapatikana getini”,amesema.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments