NAMUNGO FC WAITUNISHIA MISULI YANGA SC ...MASHABIKI WAONDOKA KWA HASIRA BAO KUKATALIWA

Vigogo Yanga SC wamelazimishwa sare ya bila mabao na wenyeji Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.

Hata hivyo mashabiki wa Yanga waliondoka na hasira uwanjani kufuatia refa Hance Mabena wa Tanga kukataa bao lao lililofungwa na mshambuliaji Mburkinabe, Yacouba Sogne kwa kichwa akimalizia mpira wa kona kipindi cha pili.

Kwa sare hiyo, Yanga SC inafikisha pointi 58 baada ya kucheza mechi 28 na inabaki nafasi ya pili, sasa ikizidiwa pointi tatu na mabingwa watetezi, Simba SC ambao pia wa mechi tatu mkononi, wakati Namungo FC yenyewe inafikisha pointi 36 baada ya mechi 26 nayo pia inabaki nafasi ya 10.

Via Binzubeiry blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments