SALOME WIG POINT TZ WANOGESHA MAONESHO YA WAJASIRIAMALI NA WAWEKEZAJI KAHAMA....TAZAMA BIDHAA ZAO HAPA

Kampuni ya Salome Wig Point Tz wanaojihusisha na utengenezaji wa Wig aina zote, kusuka mitindo yote ya nywele,kukodisha magari na kupamba maharusi inashiriki katika Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yaliyoandaliwa na Taasisi ya GS1 Tanzania kupitia Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Kahama.

Akizungumza na Malunde 1 blog leo Jumanne Mei 25,2021 Mkurugenzi wa Kampuni ya Salome Wig Point Tz, Bi. Salome Mvanga amesema wanashiriki maonesho hayo ili kuonesha na kuuza bidhaa mbalimbali wanazotengeneza.

"Salome Wig Point Tz tunapatikana  Mkabala na Gaprena Hotel Mjini Kahama na Kariakoo Jengo la JAH Plaza jijini Dar es salaam.

Tunatengeneza ma wig,  tunauza vipodozi, ma wig aina zote kwa bei ya jumla na reja reja, tunatengeneza nywele natural, vibanio vya nywele, tunafanya make up, tunasuka nywele aina zote.  Karibuni kwa huduma zote za urembo na ushauri. Mawasiliano yetu ni 0763278182",amesema Salome.

Maonesho ya Wajasiriamali na Wawekezaji Kahama yameanza Jumatatu Mei 24,2021 yakitarajiwa kufikia tamati Mei 30,2021 katika viwanja vya Kituo cha Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kilichopo Nyihogo Mjini Kahama yanaongozwa na kauli mbiu ya ‘Nunua bidhaa za Kitanzania kuza uchumi wa nchi’ yakiwapa Wajasiriamali fursa ya kuonesha na kuuza bidhaa zao.
Mfanyakazi wa Kampuni ya Salome Wig Point Tz, Bi. Magreth Paschal akionesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza na kuuza kwenye Maonesho ya Wajasirimali na Wawekezaji Kahama leo Jumanne Mei 25,2021 . Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Wafanyakazi wanKampuni ya Salome Wig Point Tz, Bi. Magreth Paschal na Elvira Richard (kushoto) wakionesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza na kuuza kwenye Maonesho ya Wajasirimali na Wawekezaji Kahama leo Jumanne Mei 25,2021 
Wafanyakazi wa Kampuni ya Salome Wig Point Tz, Bi. Magreth Paschal na Elvira Richard  (kushoto) wakionesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza na kuuza kwenye Maonesho ya Wajasirimali na Wawekezaji Kahama leo Jumanne Mei 25,2021 
Wafanyakazi wa Kampuni ya Salome Wig Point Tz, Bi. Magreth Paschal na Elvira Richars (kushoto) wakionesha bidhaa mbalimbali wanazotengeneza na kuuza kwenye Maonesho ya Wajasirimali na Wawekezaji Kahama leo Jumanne Mei 25,2021 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments