OMMY DIMPOZ AIBUKIA MAKKA


Msanii Ommy Dimpoz

Msanii Ommy Dimpoz yupo mjini Makka nchini Saudia Arabia, ameungana na waumini mbalimbali wakiislamu duniani kufanya ibada ya Umrah baada ya mwaka 2019 kushindikana kutokana na kuumwa.

Dimpoz amekuwa ni mtu wa ibada siku zote na kupitia ukurasa wake wa Instagram, ame-post picha kadhaa akiwa ndani ya msikiti jirani “Al-Ka'abah” ambao ni nyumba maalum ya Mwenyezi Mungu na kawaida wahudhuriaji huzunguka mara 7.

Makka ni mji mtakatifu wa Uislamu na kila mwaka mamilioni wa Waislamu wanahiji kwenda Makka.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments