MWIGIZAJI MREMBO MWENYE SHEPU MATATA AJARIBU KUJIUA KISA MAPENZI

Mrembo na mwigizaji mahiri kutoka nchini Ghana mwenye shepu matata, Princess Shyngle.
Mrembo na mwigizaji mahiri kutoka nchini Ghana mwenye shepu matata, Princess Shyngle.
Mrembo na mwigizaji mahiri kutoka nchini Ghana mwenye shepu matata, Princess Shyngle.
***
MREMBO na mwigizaji mahiri kutoka nchini Ghana mwenye shepu matata, Princess Shyngle amelazwa katika hospitali moja nchini Marekani baada ya kujaribu kujiua, likiwa ni jaribio lake la pili ndani ya kipindi cha miaka mitatu.


Video iliyopostiwa katika akaunti ya mtandao wa kijamii wa Instagram ya mwanadada huyo, inamuonesha akiwa ndani ya gari la kubebea wagonjwa (ambulance) akikimbizwa hospitalini huku chini ya video hiyo kukiwa na maneno ‘Depression is real’ akimaanisha msongo wa mawazo siyo kitu cha kutania.


Inaelezwa kwamba mwanadada huyo mwenye asili ya nchini Gambia, anadaiwa kutaka kujiua kwa kumeza idadi kubwa ya vidonge ambavyo bado havijafahamika ambapo aliokolewa na wasamaria wema akiwa katika hali mbaya na kukimbizwa hospitalini.


Hii ni mara ya pili kwa mrembo huyo kujaribu kujiua, mara ya kwanza ikiwa ni mwaka 2018 ambapo alimeza idadi kubwa ya vidonge sambamba na dawa ya kuondoa madoa kwa lengo la kukatisha uhai wake akiwa nchini Nigeria.


Inaelezwa kwamba jirani yake ndiye aliyemuokoa na kumkimbiza katika Hospitali ya Vedic Lifecare Hospital iliyopo Lekki nchini Nigeria.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments