AZIKWA KISHA KUFUKULIWA NA KURUDISHWA MOCHWARI KIMYA KIMYA

Linaweza kuwa tukio la ajabu, lakini ndio limetokea huku usiri mkubwa ukitawala. Ndugu wa familia ya marehemu Danielson Lema (72), aliyekuwa mkazi wa Kijiji cha Nkwansira wilayani Hai, Kilimanjaro, wamepewa maiti ya mtu mwingine, Shanshandumi Kimaro (82) na kwenda kuzika bila kubaini kuwa sio ndugu yao.

Mwili wa Kimaro, aliyekuwa mkazi wa Kijiji cha Isuki ulizikwa na familia ya Lema Mei Mosi, mwaka huu baada ya kukabidhiwa kimakosa na wahudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Hai.

Hata hivyo, Mei 2 mwili huo ulifukuliwa kisha kurudishwa kwenye chumba cha maiti kimya kimya bila uongozi wa hospitali hiyo kubaini.

Tukio hilo ambalo lilifanyika kwa usiri mkubwa, limeibua maswali mengi tata kuhusu usalama na umakini wa wahudumu wa chumba cha maiti pamoja na ndugu husika kushindwa kutofautisha miili ya wapendwa wao licha ya kuwepo kwa taratibu za ndugu kutambua mwili kabla ya kukabidhiwa.

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments