WANAUME WAPOTEZA FAHAMU BAADA YA KUIBA NGURUWE WA BIBI

Kumetokea tukio la aina aina yake huko Shinyalu, Kaunti ya Kakamega nchini Kenya baada ya wanaume wawili wanaodaiwa kuiba nguruwe wa ajuza mmoja kuanguka na kupoteza fahamu. 

Afisa Mkuu msaidizi wa polisi eneo la Shisembe Mike Shivanda amethibitisha kisa hicho kulingana na ripoti ya OB iliyowasilishwa katika Kituo cha Polisi cha Shinyalu kwamba nguruwe hao waliibiwa Aprili 17,2021 majira ya saa nne asubuhi.

"Iliripotiwa na Mike Shivanda, chifu msaidizi, eneo dogo la Shisembe, kwamba wanaume wawili walianguka na kupoteza fahamu ndani ya kijiji cha Munyolo katika eneo la Murhanda takriban kilomita sita kaskazini mwa kituo hicho. 

"Maafisa walitembelea eneo la tukio na kupata wanaume wawili, ambao ni; Nicholas Abung'ana, mwanaume wa Luhya mwenye umri wa miaka 50, na Alexander Savala, wa kiume wa Luhya mwenye umri wa miaka 50 wakiwa wamelala katika nyumba zao, hawawezi kuongea au kuamka," ripoti ilisema.

Mwanamke mzee ambaye nguruwe wake waliibwa alitambuliwa kwa jina Doris Achitsa, 65, ambaye anadaiwa kuwa mwajiri wa Abung'ana.

 Achitsa ni binamuye Savala, ambaye ni mmoja wa washukiwa ambaye alipatikana amepoteza fahamu. 

Kulingana na ripoti ya polisi kwenye kitabu cha matukio (OB), mwanamke huyo ambaye alionekana mwenye masikitiko makubwa alitafuta huduma za mganga mmoja Kaunti ya Bungoma ambaye alimtembelea nyumbani kwake majira ya saa 12 jioni na kufanya ibada zake kabla ya kuondoka ambapo ilipotimia saa 1 usiku, wanaume hao wawili walianguka na kupoteza fahamu.

 Mfuasi huyo alikuwa ameacha maagizo kwamba mtu yeyote atakayeathiriwa asichukuliwe hospitalini bali aachwe katika hali yoyote aliyokuwa nayo hadi asubuhi atakaporudi. 

Ndugu zao walisisitiza kwamba maagizo ya mfuasi wa ibada yazingatiwe. 

Ripoti ya maendeleo ya kesi ya PUI ifuatwe," iliongeza.

SOMA ZAIDI <<HAPA>>




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments