AHUKUMIWA KUTUMIKIA KIFUNGO CHA SIKU MOJA TU BAADA YA KUMUUA MME WAKE KWA PANGA


Picha Truphena Ndonga aliyemuua mumewe kwa panga
**
Mwanamke kutoka Kaunti ya Siaya nchini Kenya, Truphena Ndonga amefunguka kusema ameona miujiza wa ajabu ambao hakuutarajia baada ya kuhukumiwa kifungo cha siku moja kwa kosa la kumuua mumewe kwa Panga.

Truphena Ndonga amesema alijua maisha yake ndio yamefikia ukomo na alidhani angehukumiwa kifungo cha maisha au adhabu ya kunyongwa kutokana na kosa alilolifanya.

Akieleza chanzo cha kumuua mumewe James Oyengo kwa panga Truphena Ndonga amesema hakukusudia kufanya kitendo hicho ila mumewe alikuwa amelewa na kuanzisha ugomvi huku ameshika panga, hivyo akafanikiwa kujiteteta na kumpokonya panga mumewe kisha kumpiga nalo kama njia ya kujikinga.

Aidha ameendelea kusema kwa sasa anaishi kwa kaka yake na anaogopa kurudi nyumbani kwake kwani anajua uchungu wa upande wa ndugu wa mumewe haujaisha pia amepanga kuomba msamaha kwa familia ya mumewe.

Chanzo : Tuko News

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments