BALOZI KIJAZI KUZIKWA TANGA JUMAMOSI FEBRUARI 20

Balozi John Kijazi enzi za uhai wake

Na Aurea Simtowe - Mwanchi

 Katibu mkuu Ikulu, Dk Moses Kasiluka amesema aliyekuwa katibu mkuu kiongozi, Balozi John Kijazi atazikwa Jumamosi Februari 20, 2021 wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga.


Amesema ibada ya kuaga mwili wa Balozi Kijazi aliyefariki dunia jana Jumatano Februari 17, 2021 katika hospitali ya Benjamin Mkapa mkoani Dodoma itafanyika kesho asubuhi katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Rais John Magufuli.

Amesema leo shughuli ya kuaga mwili wa Balozi Kijazi ilifanyika katika Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) na kisha mwili ukasafirishwa hadi jijini Dar es Salaam.

“Utasafirishwa kwenda Dar es Salaam nyumbani wake na utalala hapo na kesho asubuhi kutakuwa na ibada itakayoongozwa na Rais Magufuli na viongozi wengine wa Serikali.”

“Baada ya kukamilisha shughuli ya kuaga ratiba tuliyonayo ni kuwa atazikwa siku ya Jumamosi, Korogwe nyumbani kwao, tunawakaribisha wote wanaoweza kushiriki kumsindikiza kiongozi wetu,” amesema Dk Kasiluka.

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments