Picha : KAMPUNI YA DELLAH CAR TRADERS YAKABIDHI RASMI GARI LA CHAMA CHA WALIMU MANISPAA YA SHINYANGA


Muonekano wa gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga likiwa nje ya Ofisi za CWT mkoa wa Shinyanga baada ya kuletwa na Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company leo Ijumaa Februari 5,2021.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya Uagizaji wa Magari  nje ya nchi maarufu Dellah Car Traders Company imekabidhi rasmi gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 ililoagiza kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.

Kampuni hiyo ya Uagizaji wa Magari  nje ya nchi Dellah Car Traders Company yenye makao makuu Mjini Shinyanga na tawi la Dar es salaam Magomeni Usalama Jengo la 3D imekabidhi gari hilo ililoliagiza Japan leo Ijumaa Februari 5,2021 kwa Mwenyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga, John Balele

Shangwe za walimu kupokea gari hilo zilianzia katika ofisi za Dellah Car Traders Company ambapo wamefanya maandamano wakipita katika mitaa mbalimbali mjini Shinyanga kuelekea katika ofisi cha Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) mkoa wa Shinyanga ambapo hafla fupi ya makabidhiano ya gari imefanyika.

Akizungumza wakati wa Kukabidhi gari hilo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company inayojihusisha na uagizaji magari Japan, Dubai, Singapore na UK, Edwin Charles Dellah amesema waliagiza gari hilo Japan Desemba 16,2020 na gari hiyo imefika ndani ya siku 45 ambapo imefika Dar  es salaam Januari 28, 2021 na wamekabidhi leo Februari 5,2021.

Mkurugenzi huyo amekishukuru Chama Cha Walimu Manispaa ya Shinyanga kuiamini Kampuni hiyo mama kuagiza gari hilo ambalo litatumika kwa shughuli mbalimbali za walimu.

“Tunatoa shukrani kwa Chama Cha Walimu Manispaa ya Shinyanga kwa kuiamini kampuni yetu mama ya Dellah Car Traders Company. Tulikuwa Wazabuni watatu lakini sisi tukashinda tenda ya kununua gari la CWT ambalo limegharimu jumla ya shilingi milioni 49 na laki 9”,amesema Dellah.

Mtaalamu huyo wa magari na Wakala wa uagizaji magari, amesema yupo tayari kutoa elimu kuhusu namna ya kutunza gari hilo ili liwe imara zaidi na kuhakikisha linadumu kwa muda mrefu huku akiongeza kuwa pia wamefunga TV na muziki wa kisasa katika gari hilo ili kuwapa raha zaidi walimu wa Manispaa ya Shinyanga.

Akipokea gari hilo, Mwenyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga, John Balele amesema gari hilo ni zuri na injini yake ni nzuri akibainisha kuwa gari hilo siyo kwa ajili ya viongozi wa CWT bali litatumika kwa ajili ya walimu wote bila ubaguzi wa aina yoyote.

“Wengi hawakuamini kama Dellah Car Traders  Company wangeleta gari zuri lakini ukweli ni kwamba wameleta gari zuri. Tumefurahi gari tuliloagiza ndiyo gari waliloleta. Mchakato wa kununua gari hili ulikuwa mgumu sana, tulikuwa na Wazabuni watatu. Tunawapongeza Dellah kutuletea gari zuri. Dellah, kamati ya manunuzi na kamati tendaji ya CWT mmetuheshimisha”,amesema Balele.

Aidha ametumia fursa hiyo kuwataka walimu kutunza gari na kuepuka kutozozania gari hilo  na watengeneze kanuni za kuendeshea gari hilo na kuhakikisha linatumika kwa shughuli za walimu siyo kwa malengo ya biashara vinginevyo litawapa shida

Naye Mwenyekiti wa CWT Manispaaa ya Shinyanga, Meshack Mashigala amesema gari hilo litatumika kusaidia walimu katika  shida na raha akieleza kuwa walimu walikuwa wanapata changamoto kubwa ya usafiri pindi wanapopatwa na matatizo.

“Pongezi nyingi ziwafikie walimu wa Manispaa ya Shinyanga ambao wana mategemeo makubwa katika gari hili ambapo sasa shida zao zitaisha”,amesema Mashigala.

Awali akisoma taarifa ya ununuzi wa gari la CWT Manispaa ya Shinyanga, Katibu wa CWT Manispaa ya Shinyanga, James Msimbang’ombe amesema waliingia mkataba na Kampuni ya Dellah Car Traders Company kununua gari Novemba 25,2020 kwa gharama ya shilingi milioni 49.9 ambapo Kampuni hiyo imeleta gari hilo ndani ya siku 45.

Muonekano wa gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga likiwa nje ya Ofisi za CWT mkoa wa Shinyanga baada ya kuletwa na Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company leo Ijumaa Februari 5,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu wa CWT Manispaa ya Shinyanga, James Msimbang’ombe akisoma taarifa ya ununuzi wa gari la CWT Manispaa ya Shinyanga,  amesema waliingia mkataba na Kampuni ya Dellah Car Traders Company kununua gari Novemba 25,2020 kwa gharama ya shilingi milioni 49.9 ambapo Kampuni hiyo imeleta gari hilo ndani ya siku 45.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company inayojihusisha na uagizaji magari Japan, Dubai, Singapore na UK, Edwin Charles Dellah akikishukuru Chama Cha Walimu Manispaa ya Shinyanga kwa kuiamini Kampuni hiyo kuwaagizia gari Japan Desemba 16,2020 na gari hiyo imefika ndani ya siku 45 ambapo iliwasili  Dar  es salaam Januari 28, 2021 na wamekabidhi leo Februari 5,2021.
wenyekiti wa CWT Manispaaa ya Shinyanga, Meshack Mashigala akizungumza wakati wa kupokea gari hilo ambapo amesema gari hilo litatumika kusaidia walimu katika  shida na raha akieleza kuwa walimu walikuwa wanapata changamoto kubwa ya usafiri pindi wanapopatwa na matatizo.
Mwenyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga, John Balele akizungumza wakati wa kupokea gari aina ya Toyota Coaster ambapo amesema gari hilo ni zuri na injini yake ni nzuri akibainisha kuwa gari hilo siyo kwa ajili ya viongozi wa CWT bali litatumika kwa ajili ya walimu wote bila ubaguzi wa aina yoyote.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company, Edwin Charles Dellah akielezea kuhusu usajili wa gari aina ya Toyota Coaster kwa ajili ya Chama Cha Walimu Manispaa ya Shinyanga wakati akikabidhi nyaraka za manunuzi ya gari.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company inayojihusisha na uagizaji magari Japan, Dubai, Singapore na UK, Edwin Charles Dellah akimkabidhi Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Shinyanga, Lazaro Saulo nyaraka za ununuzi wa gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ ikiwa na  thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company inayojihusisha na uagizaji magari Japan, Dubai, Singapore na UK, Edwin Charles Dellah akimkabidhi Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Shinyanga, John Balele nyaraka za ununuzi wa gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa CWT Mkoa wa Shinyanga, John Balele akiwakabidhi Viongozi wa CWT Manispaa ya Shinyanga nyaraka za ununuzi wa gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga, John Balele akizindua gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa kulimwagia maji kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Mmoja wa wafanyakazi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company akibandua kibao cha Dellah Car Traders Company ili kibao cha gari aina ya Coaster chenye namba za usajili T 682 DVJ kionekane. 
Kibao cha gari aina ya Toyota Coaster kikionesha namba za usajili T 682 DVJ baada ya kibao cha Dellah Car Traders Company kubanduliwa.
Walimu na wafanyakazi wa Dellah Car Traders Company wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company inayojihusisha na uagizaji magari Japan, Dubai, Singapore na UK, Edwin Charles Dellah akiwasha muziki ndani ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Baadhi ya walimu wakiwa ndani ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
 Mwenyekiti wa CWT mkoa wa Shinyanga John Balele (kushoto) akimpongeza Mkurugenzi wa Kampuni ya Dellah Car Traders Company inayojihusisha na uagizaji magari Japan, Dubai, Singapore na UK, Edwin Charles Dellah kwa ununuzi wa gari nzuri aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Muonekano wa gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga likiwa nje ya Ofisi za CWT mkoa wa Shinyanga baada ya kuletwa na Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company leo Ijumaa Februari 5,2021.
Shangwe zikitawala baada ya makabidhiano ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga nje ya Ofisi za CWT mkoa wa Shinyanga baada ya kuletwa na Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company leo Ijumaa Februari 5,2021.
Muonekano wa gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga
Wafanyakazi wa Dellah Car Traders Company wakipiga picha ya kumbukumbu baada ya kukabidhi gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Wafanyakazi wa Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company na viongozi wa CWT wakipiga picha ya kumbukumbu
Awali gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga likiwa nje ya Ofisi za Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company leo Ijumaa Februari 5,2021.
Muonekano wa bango nje ya ofisi za Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company katika jengo la Seif Hotel Mjini Shinyanga.
Maandamano yakiendelea mjini Shinyanga wakati wa zoezi la makabidhiano ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Maandamano yakiendelea mjini Shinyanga wakati wa zoezi la makabidhiano ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Maandamano yakiendelea mjini Shinyanga wakati wa zoezi la makabidhiano ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Maandamano yakiendelea mjini Shinyanga wakati wa zoezi la makabidhiano ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ yenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Maandamano yakiendelea mjini Shinyanga wakati wa zoezi la makabidhiano ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga.
Maandamano yakiendelea mjini Shinyanga wakati wa zoezi la makabidhiano ya gari aina ya Toyota Coaster yenye namba za usajili T 682 DVJ lenye thamani ya shilingi milioni 49.9 kwa ajili ya Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) Manispaa ya Shinyanga baada ya kuletwa na Kampuni ya Uagizaji Magari ya Dellah Car Traders Company leo Ijumaa Februari 5,2021.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments