Tanzia : KATIBU MKUU WA KKKT DAYOSISI YA KASKAZINI ARTHUR SHOO AFARIKI DUNIA


Katibu mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) yenye makao yake makuu mjini Moshi, Arthur Shoo enzi za uhai wake
Katibu mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) yenye makao yake makuu mjini Moshi, Arthur Shoo
***
Katibu mkuu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) yenye makao yake makuu mjini Moshi, Arthur Shoo amefariki dunia katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC alikokuwa akipatiwa matibabu.

Mkuu wa Dayosisi hiyo ambaye ndiye mkuu wa Kanisa hilo Tanzania, Askofu Fredrick Shoo amesema kuwa mtendaji wake huyo mkuu alifariki dunia jana usiku akiendelea na matibabu hospitali ya KCMC na kueleza kuwa alikuwa amelazwa katika hospitali hiyo inayomilikiwa na Shirika la Msamaria Mwema (GSF) tangu Jumatatu ya wiki hii.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments