MLEZI WA SKAUTI MIKOA YA NYANDA ZA JUU KUSINI AFANYA ZIARA MKOANI MBEYA

 

Kamishna Mkuu Msaidizi wa Skauti Tanzania anayeshughulikia makambi na mazingira ambaye pia ni mlezi wa mikoa ya  Nyanda za Juu Kusini ya Mbeya, Ruvuma na Iringa, Mary Anyitike.
Kamishna Mkuu Msaidizi wa Skauti Tanzania anayeshughulikia makambi na mazingira ambaye pia ni mlezi wa mikoa ya Mbeya, Ruvuma na Iringa, Mary Anyitike akisalimiana na Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock Ntole baada ya kuwasili mkoani Mbeya.
Kamishna Mkuu Msaidizi wa Skauti Tanzania anayeshughulikia makambi na mazingira ambaye pia ni mlezi wa mikoa ya Mbeya, Ruvuma na Iringa, Mary Anyitike akisaini kitabu cha wageni. Kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Skauti Wilaya ya Chunya, Mwalimu Alex Nyangwa na kulia ni Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock Ntole.
Kamishna Mkuu Msaidizi wa Skauti Tanzania anayeshughulikia makambi na mazingira ambaye pia ni mlezi wa mikoa ya Mbeya, Ruvuma na Iringa, Mary Anyitike (katikati) akiwa na viongozi wa Skauti Mkoa wa Mbeya. Kulia ni Kamishna Msaidizi wa Skauti Wilaya ya Chunya, Mwalimu Alex Nyangwa na kushoto ni Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock Ntole.
Kamishna Mkuu Msaidizi wa Skauti Tanzania anayeshughulikia makambi na mazingira ambaye pia ni mlezi wa mikoa ya Mbeya, Ruvuma na Iringa, Mary Anyitike (katikati) akiwaelekeza jambo viongozi wa Skauti Mkoa wa Mbeya. Kulia ni Kamishna Msaidizi wa Skauti Wilaya ya Chunya, Mwalimu Alex Nyangwa na kushoto ni Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock Ntole

Mjumbe wa Bodi wa Skauti, Christopher Mwasambili (kulia) akizungumza kwenye kikao cha bodi.

Mwenyekiti wa Bodi wa Skauti, Dkt.Julius Kaijage (kushoto) akiwa na Kamishna Mkuu Msaidizi anayeshughulikia Makambi na Mazingira, Mary Anyitike  (katikati) na Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock Ntole.
 Kamishna Mkuu Msaidizi anayeshughulikia Makambi na Mazingira, Mary Anyitike, akikagua eneo la uwanja wa Skauti mkoani humo.
Kamishna Mkuu Msaidizi anayeshughulikia Makambi na Mazingira, Mary Anyitike, akizungumza na wananchi na wafanya biashara ndogo ndogo wanaoishi jirani na uwanja huo . 
Wananchi na wafanyabiashara ndogo ndogo wanaoishi jirani na uwanja huo .wakimsikilza Kamishna Mkuu Msaidizi anayeshughulikia Makambi na Mazingira, Mary Anyitike (hayupo pichani)

Na Dotto Mwaibale, Mbeya

KAMISHNA Mkuu Msaidizi wa Skauti Tanzania anayeshughulikia makambi na mazingira ambaye pia ni mlezi wa mikoa ya Mbeya, Ruvuma na Iringa, Mary Anyitike amefanya ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Mbeya.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa juzi, Anyitike alisema kuwa lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kuangalia utendaji kazi na kutembelea Uwanja wa Skauti  wa Ally Hassan Mwinyi uliopo  mkoani humo.

" Lengo la ziara hii ya siku moja ilikuwa ni kuangalia utendaji kazi na kutembelea uwanja wetu ambapo   pia  nilipata nafasi ya kuzungumza na baadhi ya wajumbe wa bodi ya skauti mkoani hapa na kuhudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi wa Skauti, Dkt.Julius Kaijage." alisema Anyitike.

Aidha Anyitike alisema kuwa katika ziara hiyo alipata fursa ya kuzungumza na wananchi wanaoishi jirani na uwanja huo na wafanya biashara ndogo ndogo  kwa lengo la kujua changamoto zinazowakabili ili kuzipatia ufumbuzi na kudumisha ujirani mwema.

Kamishna wa Skauti Mkoa wa Mbeya, Sadock Ntole alisema ziara hiyo ya kikazi ya Anyitike imewapa mori zaidi wa kazi  na kuwa ujumbe walioupata ataufikisha katika wilaya zote za mkoa huo.

"Tumefarijika sana na ziara ya mlezi wetu na yote aliyotuelekeza tutayafanyia kazi" alisema Ntole.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments