YANGA BINGWA MAPINDUZI CUP, YAICHAPA SIMBA SC KWENYE MIKWAJU YA PENALTI 4-3


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduziu Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi Kombe la Ubingwa wa Michuano ya Mapinduzi Cup Nahodha wa Timu ya Yanga Haruna Nyonzima, baada kuifunga Timu ya Simba katika mchezo wa Fainali uliofanyika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)

********************
Na Emmanuel Mbatilo - Zanzibar
Klabu ya Yanga imefanikiwa kunyakua ubingwa wa Mapinduzi Cup baada ya kuinyuka katika mikwaju ya penalti baada ya kutoka sare ya bila kufungana ndani ya dakika 90 za mchezo.

Nyota wa mchezo huo ni Farouk Shikalo ambaye aliokoa penalti moja ya Joash Onyango na Meddie Kagere kugongengesha mwamba penalti yake moja.

Saido Ntibanzokiza ambaye alikuwa msumbufu ndani ya dakika zote 90 amesema kuwa wachezaji wenzake walimuomba awape sapoti naye akasema kwamba hana tatizo atafanya kazi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments