TETESI ZA SOKA LEO ALHAMISI JANUARI 7,2021



Mazungumzo mapya ya kandarasi kati ya Liverpool na kiungo wa kati wa Uholanzi Georginio Wijnaldum, 30, yamegonga. (Sky Sports).

Mgombea wa rais katika klabu ya Barcelona Agusti Benedito anasema kwamba hafikirii kwamba Lionel Messi 33 ataongeza mtakaba wake katika klabu hiyo unaoisha mwezi Juni 2021. (Goal)

Manchester City inaamini wako mbele ya mstari kumsaini lionel Messi iwapo mshambuliaji huyo wa Argentina ataondoka Barcelona katika majira ya joto. (Telegraph - subscription required)
Lakini Barcelona inasema kwamba itajaribu kuzungumza na Messi ili kumshawishi kuongeza mkataba wake baada ya kusema kwamba angependelea kucheza nchini Marekani mwisho wa mchezo wake. (AS)

Everton inataraji kupokea ofa za Moise Keane 20 kutoka klabu ya PSG , ambapo mshambulaji huyo wa Itali yuko katika mkopo lakini pia Everton haina haraka kuamua kuhusu hatma yake ya baadae.. (Liverpool Echo)

Kiungo wa kati wa Arsenal na Ujerumani Mesut Ozil, 32, amekubali mkataba wa miaka mitatu na nusu na klabu ya uturuki Fenerbahce. (DHA - in Turkish
Hatima ya Ozil itaamuliwa hivi karibuni , lakini lengo la mshindi huyo wa kombe la dunia ni kusalia Arsenal hadi kandarasi yake itakapokamilika katika majira ya joto.. (ESPN)

CHANZO - BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments