SAVE THE CHILDREN YAENDESHA MDAHALO WA BAJETI JUMUISHI NGAZI YA HALMASHAURI MANISPAA YA SHINYANGA


Mtaalam wa Haki za Watoto na Utawala Bora kutoka Save The Children Makao Makuu Jesca Ndana, akizungumza kwenye Madahalo huo.

Na Marco Maduhu  Shinyanga. 

Shirika la Save The Children linalojihusisha na utetezi wa haki za watoto katika nchi 117 duniani ikiwemo Tanzania, limeendesha mdahalo wa utekelezaji wa bajeti jumuishi katika sekta zinazomuhusu mtoto moja kwa moja katika halmashauri ya manispaa ya Shinyanga.

Mdahalo huo umefanyika leo, katika ukumbi wa Hoteli ya Empire Mjini Shinyanga, ambao umekutanisha maafisa elimu, maendeleo, wachumi, viongozi wa kisiasa, dini, wajumbe wa baraza la watoto, wadau kutoka mashirika na asasi zisizo za kiserikali, waandishi wa habari, pamoja na maofisa kutoka TAMISEMI wanaohusika na masuala ya bajeti, huku mgeni rasmi akiwa ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Geoffrey Mwangulumbi. 

Mratibu wa Mradi wa Mijadala Jumuishi katika Masuala ya Uchumi na Utawala wa Kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, amesema wameandaa na kuwezesha mdahalo huo ,ili wadau wajadili kwa pamoja namna ya kupanga bajeti bora ambayo itazingatia maslahi mapana ya watoto. 

Amesema Shirika hilo limekuwa likitekeleza miradi mbalimbali ya utetezi wa haki za watoto ikiwemo mradi huu wa mijadala jumuishi, ambao utekelezaji wake ulianza mwaka jana (2020), na umelenga zaidi masuala ya kisera ya utekelezaji wa bajeti zinazomhusu mtoto na utakoma mwaka huu (2021).

Ameongeza kuwa kupitia mradi huu Save the Children ingependa kuona ushirikishwaji wa wadau wakiwemo wanajamii wa kawaida na watoto katika mchakato wa kibajeti na kuboresha utekelezaji wa bajeti za watoto. 

"Save the Children tumeendesha mdahalo huu wa bajeti jumuishi haswa tukianzia sekta inayomgusa mtoto moja kwa moja, kwa lengo la kujadiliana namna ya kupanga bajeti ambayo itazingatia maslahi ya watoto katika sekta hizo mbazo ni afya na lishe, elimu, maendeleo ya jamii, ulinzi na usalama wa mtoto," amesema Enock. 

"Mradi huu unatekelezwa katika wilaya tano zikiwemo Unguja mjini, Magharabi “A” na “B” Visiwani Zanzibar, na wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, pamoja na manispaa ya Shinyanga, kwa ufadhili wa Umoja wa Ulaya (EU).

"Ni matarajio yetu kuwa wadau kwa kushirikiana na halmashauri husika zitaweza kuyapa kipaumbele masuala ya watoto kwenye bajeti zao, na hivyo kumuwezesha mtoto wa Kitanzania kupata haki zake", ameongeza. 

Kwa upande wake mgeni rasmi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Geoffrey Mwangulumbi, amelipongeza Shirika la Save the Children kwa kuendesha mdahalo huo, na kubainisha upo katika muda muafaka, ambapo wadau wanapaswa kuanza kujadili kuanzia sasa vipaumbele na malengo ya bajeti ngazi za chini. 

Amesema katika upangaji wa bajeti hizo ikiwamo ya watoto, kuwepo na vipaumbele vichache muhimu, ambavyo vitaweza kutekelezeka kulingana na bajeti ya fedha za halmashauri, kuliko kuwa na vipaumbele vingi ambavyo haviwezi kutekelezeka. 

Naye Makamu Mwenyekiti Baraza la watoto Manispaa ya Shinyanga Nancy Kasembo, amepongeza mdahalo huo, ambao umewapatia mwanga wa namna ya kushiriki kikamilifu kwenye utoaji wa mapendekezo ya bajeti zinazomhusu mtoto. 

TAZAMA PICHA HAPA CHINI
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Geofrey Mwangulumbi, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Mratibu wa mradi wa mijadala jumuishi katika masuala ya uchumi na utawala wa kifedha Alex Enock kutoka Shirika la Save The Children mkoani Shinyanga, akiendelea kuzungumza kwenye Mdahalo huo.
Mtaalamu wa haki za watoto na utawala Bora kutoka Save The Children Makao Makuu Jesca Ndana, akizungumza kwenye Madahalo huo.
Mtaalam wa Haki za watoto na utawala Bora kutoka Save The Children Makao Makuu Jesca Ndana, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Mchumi kutoka TAMISEM Allan Bendera, akizungumza kwenye Mdahalo huo.
Gerald Ng'ong'a ambaye alikuwa mwenyekiti wa Mdahalo huo akizungumza na kutoa maoni yake.
Washiriki wakiwa kwenye Mdahalo huo.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Mdahalo ukiendelea.
Waandishi wa Habari nao wakishiriki kwenye Mdahalo huo, wakwanza kushoto ni Fanki Mshana Mwandishi wa ITV, katika Suzy Butondo wa Mwananchi, akifuatiwa na Malaki Philipo wa RFA.
Diwani wa Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga Mussa Elias akichangia mada kwenye Mdahalo huo.
Mchumi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Gwakisa Mwasheba, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akichangia Mada kwenye Mdahalo huo
Mwenyekiti wa Shirikisho wa vyama vya watu wenye ulemavu mkoani Shinyanga (SHIVYAWATA), Richard Mpongo, akichangia mada kwenye Mdahalo huo.
John Shija kutoka Shirika la PACESH Mkoani Shinyanga akichangia mada kwenye Mdahalo huo.
John Eddy kutoka Shirika la TAWLAE, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Makamu Mwenyekiti Baraza la watoto Manispaa ya Shinyanga Nancy Kasembo, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Mchumi kutoka TAMISEM Allan Bendera, akichangia Mada kwenye Mdahalo huo.
Washiriki wa Mdahalo huo wakiwa kwenye kazi ya vikundi.
Kazi ya vikundi ikiendelea.
Kazi ya vikundi ikiendelea.
Kazi ya vikundi ikiendelea.
Uwasilishaji kazi ya vikundi ukiendelea.
Uwasilishaji kazi ya vikundi ukiendelea.
Uwasilishaji kazi ya vikundi ukiendelea.

Na Marco Maduhu- Shinyanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments