RAIS YOWERI MUSEVENI AMTEUA MWANAJESHI KURATIBU MASUALA YA USALAMA UGANDA


Rais Yoweri Museveni wa Uganda amemteua meja generali Kayanja Muhanga kuwa mratibu wa masuala ya usalama nchini Uganda.

Naibu msemaji wa jeshi luteni kanali Deo Akiiki ameambia BBC kwamba meja jenerali Muhanga atakuwa mratibu wa operesheni za vitengo vyote vya usalama.

‘Ni kweli kwamba Brigedia Kayanja Muhanga amepewa nafasi ya kuratibu vikundi vyote vya usalama kwa madhumuni ya kuunganisha shughuli ya usalama wa pamoja hususan katika mji wa Kampala na nchi yote’ .

"Hiyo ina maana kwamba atakuwa kiunganishi kati ya kikosi cha polisi , jeshi na idara ya ujasusi , alithibitisha luteni huyo.

CHANZO - BBC SWAHILI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments