AJIFUNGUA KANISANI KWENYE MKESHA WA MWAKA MPYA 2021 MWANZA

Na Daniel Makaka - Mwananchi
 Priska Isaya (33) makazi wa kijiji cha Kanyala wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza amejifungua mtoto wa kike akiwa anahudhuria ibada ya mwaka kwenye Kanisa ya AICT jana. 

Akizungumzia tukio hilo kanisani hapo, mchungaji wa kanisa hilo Isaka Yasini amesema mwanamke huyo alifikia kanisa kuhudhuria ibada hiyo huku ikiwa ni mara yaka ya kwanza. 

Amesema alipokuwa akiongoza ibaada hiyo alimuona mama huyu akiwa amekaa chini na alipofika kumuuliza alimwambia anaumwa uchungu.

Asema wakiwa kwenye harakati za kuona namna ya kumpeka zahanati kupata hudumua mama huyu ilichukuwa dakika tano ajifungulia kanisani na hali yake inaendelea vizuri.

Mmoja wa wanawake waliomsaidia Priska aliyejitambulisha kwa jina la Kefreni Barnaba amesema alitumia dakika tatu kufuata uzi duka liliko karibu na kanisa hilo kwa ajili ya kumufunga kitovu mtoto aliyezaliwa .

Amesema kutokana na tukio hilo Mungu ana makusudi yake hivyo tunapaswa kumshukuru kwa kila kila Jambo na kuwataka wananchi kusali kwa bidii. 

Akisimulia tukioa hilo Priska amesema kuwa yeye baada ya kupata ujauzito mume aliyempa alimkimbia na kwa sasa hajulikani aliko.

Baaada kuona hivyo aliishi maisha ya kutangatanga akiwa kisiwa cha Kasalazi kilichopo katika ziwa Victoria, huku akiomba msaada kwa wasamaria mema kutokana na maisha magumu aliyokuwa nayo baada ya kukimbia na mume.

Mwanamke huyo aliyesema amebadilisha jina lake kutoka Hadija Abubakari na kutumia jina la Priska Isaya amesema Desemba 31, 2000 alivuka kutoka kisiwa cha Kasalazi kilichopo ziwa Victoria na kwenda Kijiji cha Kanyala.

Amesema akiwa huko alikwenda kanisani lengo lilikuwa kuomba msaada na alipofika uchungu ulianza kuuma na kujifunza akiwa kanisani.

"Nyumbani kwetu ni Kagera Wilaya ya Muleba ndiko aliko mama yangu, baba yangu aliishafariki,” amesema Priska. 

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kanyala Gacha Paul amesema baada ya kupata taarifa kutoka kwa mchungaji alifika kanisani hapo na kuwashukuru wote waliotoa msaada kwa mtu huyo ambapo waliokoa maisha yake na kuitaka jamii kuwasaidia kwa kila jambo.

Kwa sasa Priska amehifadhiwa kwa mama Kefrini Barnaba akipatiwa hudumu huku waumini wa kanisa hilo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments