SIMBA SC YAACHANA NA KOCHA WAKE MKUU SVEN VAN DENBROECK


Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Simba, Sven Vandenbroeck

Na Damian Masyenene
KLABU ya Simba ya Jijini Dar es Salaam leo Januari 7, 2020 imethibitisha kuachana na Kocha wake Mkuu, Mbelgiji Sven Van Denbroeck baada ya kuwa nae kwa misimu miwili na kufanikiwa kutwaa mataji matatu ambayo ni Ligi Kuu, Kombe la Shirikisho (FA) na Ngao ya Jamii.

Taarifa hiyo inakuja ikiwa ni siku moja tu baada ya Kocha huyo kuisaidia timu hiyo kutinga hatua ya makundi ya michuano ya Klabu Bingwa barani Africa (CCL) baada ya kuichapa timu ya Platinum FC ya Zimbabwe kwa mabao 4 kwa 0 jana katika uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.


Soma zaidi taarifa ya Klabu ya Simba hapa chini


Kocha Sven Vandenbroeck (pichani) enzi zake akiwa katika majukumu yake ya kukinoa kikosi cha Simba.

Kocha huyo raia wa Ubelgiji aliiongoza Simba katika mchezo wake dhidi ya Fc Platinum ya Zimbabwe na kushinda kwa jumla ya bao 4-1 matokeo yaliyowavusha hadi hatua ya makundi ligi ya mabingwa Afrika.

TAKWIMU ZA SVEN NDANI YA SIMBA

Mechi-55

Ushindi-39

Sare-10

Vipigo-6

Mataji ya VPL-1

FA-1

Ngao ya Jamii-1

Kocha bora wa mwaka 2020

Makundi ya CAFCL

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments