Angalia Picha : MUONEKANO WA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA CHATO MKOANI GEITA


Hospitali ya Rufaa ya Kanda -Chato mkoani Geita ambayo imewekwa jiwe la msingi na Rais wa Jamhuri ya Msumbiji na Mwenyekiti wa SADC Mhe. Filipe Jacinto Nyusi mara baada ya kuwasili Chato mkoani Geita leo tarehe 11 Januari 2021.

Ujenzi wa Hospitali ya Kanda ya Chato umekamilika kwa asilimia 90 katika awamu ya kwanza ambayo makabidhiano ya miundo mbinu ya awamu hiyo ya kwanza yamepangwa kufanyika mapema mwezi Machi.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Dorothy Gwajima wakati wa uwekaji jiwe la msingi la Hospitali hiyo ya Ukanda wa Chato lililowekwa na Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi.

Dk Gwajima amesema hospitali hiyo ikikamilika itakuwa nauwezo wa kuhudumia wananchi milioni 14 kutoka Mikoa ya Kagera, Kigoma, Tabora, Rukwa, Geita, na wilaya za Mikoa ya Mwanza na Shinyanga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments