BABA ATUHUMIWA KUBAKA MTOTO WAKE WA MIAKA 11....ANASWA AKIWA NAYE 'LIVE' UCHI WA MNYAMA



Na Anthony Mayunga - Mwananchi
 Polisi wilaya ya Serengeti mkoani Mara inamshikilia mkazi wa kitongoji cha Chamoto, Ikwabe Gibogo (58) kwa tuhuma za kumwingilia kimwili mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka (11).

Mwenyekiti wa kitongoji hicho, Chacha Nyambuche amekiri mtuhumiwa kukamatwa  Januari 23,2021 usiku baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema na kumkuta nyumbani kwake amelala chini pamoja na mtoto huyo wote wakiwa hawajavaa nguo.

Mmoja wa majirani amesema mtoto huyo ameingiliwa kwa muda mrefu na baada ya kujiridhisha waliamua kutoa taarifa kwa kiongozi wa kitongoji na polisi walipofika waliwapa ushirikiano.

“Huyo mtoto hajaanza shule mpaka sasa, mama yao aliachana na baba yao baada ya kubaini anamuingilia mtoto wake mkubwa. Aliondoka na watoto wadogo kwenda Simiyu, hata hivyo, alifariki dunia ndipo mtuhumiwa akafuata watoto na kuja kuishi nao,” amesema jirani huyo kwa sharti la kutotajwa jina.

Via Mwananchi


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments