WATOTO WATATU WAFARIKI DUNIA KIGOMA BAADA YA NYUMBA KUTEKETEA KWA MOTO


Wototo wawili wa familia moja wamefariki dunia katika kijiji cha Nyarugisu wilayani Kasulu mkoani Kigoma, baada ya nyumba waliyokuwa wakiishi kuteketea kwa moto.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kigoma, -James Manyama amewataja watoto hao kuwa ni Yumwema Festo na Enifa Festo ambao ni raia kutoka nchi jirani.

Kamanda Manyama amesema kuwa, Jeshi la polisi mkoani Kigoma linaendelea kuwatafuta wazazi wa watoto hao wanaodaiwa kukimbia baada ya tukio hilo, kwa hofu ya kukamatwa kwa kosa la kuishi nchini kinyume cha sheria.

Pia amethibitisha kufariki dunia katika ajali ya moto mtoto mwingine katika kijiji cha Mpeta wilayani uvinza, baada ya nyumba alimokuwa akiishi na Wazazi wake kuungua moto.

Kufuatia matukio hayo, Kamanda Manyama amewataka Wazazi na Walezi mkoani humo kuacha utamaduni wa kuwaacha watoto nyumbani bila uangalizi.

Katika hatua nyingine Jeshi la polisi mkoani Kigoma limewataka Wakazi wa mkoa huo kusherekea sikukuu ya mwaka mpya kwa amani na kuepuka kujihusisha na vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments