Ajali yachukua uhai wa Mama wa MC Pilipili


Mama mzazi wa mshereheshaji Emmanuel Matebe maarufu kama MC Pilipili, Mariam Matebe amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Desemba 20, 2020, kwa ajali ya gari wakati akielekea ukumbini kwenye harusi ya mtoto wake maeneo ya Afrikana Jijini Dar es Salaam.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram MC Pilipili ameandika maneno haya, “Ulale salama mama yangu mpenzi Mariam Matebe, umetufundisha upendo na umefariki ukijariibu kuonesha upendo lala salama mpenzi“.

Kwa mujibu wa familia mwili wa marehemu Mama MC Pilipili  utasafirishwa leo jioni kuelekea nyumbani kwa marehemu Jijini Dodoma kwa ajili ya taratibu za maziko.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments