WAZIRI MKUU MSTAAFU WA SUDAN AFARIKI KWA CORONA


Waziri mkuu wa zamani wa Sudan, Sadiq al-Mahdi amefariki dunia kutokana na virusi vya corona.Mwanasiasa huyo amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu.

Mahdi aliyefariki akiwa na umri wa miaka 84, ndiye waziri mkuu wa mwisho wa Sudan kuchaguliwa kidemokrasia kabla ya kuondolewa madarakani mwaka 1989 kwa mapinduzi ya kijeshi yaliyomuingiza mamlakani rais wa zamani Omar al-Bashir.

Chama chake cha Umma chenye siasa za wastani, kilikuwa moja ya vyama vikubwa vya upinzani na Mahdi alisalia kuwa kiongozi mwenye ushawishi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post