Taarifa Kwa Umma Kuhusu Kuapishwa Kwa Wabunge Wapya Wateule Wa Rais


Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai leo jioni atawaapisha wabunge wawili walioteuliwa Jumapili iliyopita na Rais Dkt. John Magufuli.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kitengo cha mawasiliano cha Bunge hafla hiyo itafanyika saa 10 jioni kwenye viwanja vya Bunge, Dodoma.

Wabunge watakao apishwa na Spika Ndugai ni pamoja na Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM- NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole na Riziki Lulida ambaye alikuwa mbunge wa viti maalum kwenye Bunge la 11 kwa tiketi ya CUF.


 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments