RAIS MAGUFULI AMUAPISHA WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA


 Rais  Magufuli amemuapisha Kassim Majaliwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania baada ya kuteuliwa Novemba 12, 2020 na kuthibitishwa na wabunge ambao walipiga kura ya ndiyo  kwa asilimia 100.

Pia amewaapisha Dk Philip Mpango kuwa Waziri wa Fedha na Mipango na Profesa Palamagamba Kabudi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki.

Hafla hiyo ya kuwaapisha wasaidizi wake hao imefanyika leo Novemba 16, 2020, Ikulu Chamwino jijini Dodoma huku ikihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na wastaafu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments