MTATURU AANZA KUTEKELEZA AHADI ZA WANANCHI KWA KASI YA 4G

 

Wachungaji na waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kiaskofu Msalaba Mrefu mjini Singida, wakiwa na pikipiki walizokabidhiwa hivi karibuni na Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu kwa ajili ya kazi za kanisa hilo,
Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mkuu wa Jimbo la Kusini Usharika wa Issuna, Mchungaji, Obedi Msele.
Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mchungaji Joyce Madadi wa Usharika wa Ikungi.
 Mbunge wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu, akimkabidhi pikipiki, Mchungaji, Felix Kibiriti.


Na Dotto Mwaibale, Singida.

MBUNGE wa Singida Mashariki, Miraji Mtaturu ameanza kutekeleza ahadi zake kwa wananchi kwa kasi ya 4G.

Mtaturu ametekeleza ahadi yake  kwa kutoa pikipiki tano kwa Usharika wa Kiaskofu Msalaba Mrefu mjini Singida ambazo alimkabidhi Mchungaji Felix Kibiriti kwa niaba ya Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kati Dkt. Alex Mkumbo kwa ajili ya matumizi ya shughuli mbalimbali za kanisa hilo mkoani Singida.

Mbali ya kukabidhi pikipiki hizo zenye thamani ya sh.milioni 11, Mtaturu pia alimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo pikipiki mbili zenye thamani ya sh.milioni 4.6 kwa ajili ya Kituo cha Polisi cha Wilaya hiyo ili ziweze kusaidia kwa kazi.

Akizungumza hivi karibuni katika hafla ya kukabidhi pikipiki hizo Mtaturu alisema utoaji wa pikipiki hizo ni kutimiza ahadi yake aliyoitoa kusaidia kanisa hilo kupata usafiri wa uhakika kwa watumishi wake wanapo kwenda kuhubiri neno la Mungu.

 "Nitaendelea kutimiza ahadi zangu na kushirikiana na wananchi kwa kasi ili kuunga mkono jitihada ya Rais Dkt. John Magufuli ya kutekeleza miradi ya maendeleo" alisema Mtaturu.

Aidha Mtaturu alisema kuwa pikipiki hizo zitatumika katika sharika za Mang'onyi, Issuna, Mungaa na Ikungi zilizopo Jimbo la Singida Mashariki.

 Mtaturu alitoa ahadi hiyo Novemba 8, 2020 wakati akizindua kitabu cha Misemo na Methali za Wanyaturu kilichoandikwa na Mchungaji Dkt.Syprian Yohana Hilinti (PhD) kilichozinduliwa katika Kanisa Kuu la Kiinjili la  Kilutheri Tanzania (KKKT) Singida mjini na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwepo Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dkt.Rehema Nchimbi huko mshereheshaji katika hafla ya  uzinduzi wa kitabu hicho akiwa ni Mbunge wa Iramba  Mwigulu Nchemba.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments