DIWANI MTEULE AFARIKI DUNIA KWA KUANGUKA



 Diwani mteule wa kata ya Kinuni iliyopo Zanzibar, Suleiman Mohamed Hassan (CCM) amefariki dunia.

Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi wa CCM kwa upande wa Zanzibar, Catherine Peter Nao amesema diwani huyo alifariki ghafla juzi baada ya kuanguka nyumbani kwake na kupelekwa katika Hospitali ya Altabib.

Hassan alifariki dunia muda mfupi baadaye akiwa katika hospitali hiyo.

“Sisi kama CCM tumepokea kwa masikitiko taarifa ya msiba wa diwani Hassan na tunaiomba familia yake kuwa na moyo wa subira,” amesema Nao.

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments