RAIS MAGUFULI AMPA POLE ZITTO KABWE BAADA YA KUPATA AJALI


Rais     Magufuli, amempigia simu mgombea ubunge wa jimbo la Kigoma mjini, Zitto Kabwe, kwa lengo la kumjulia hali na kumtakia heri ili apone haraka baada ya hapo jana kupata ajali ya gari na kupata majeraha kadhaa.

Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba 7, 2020, na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, kupitia ukurasa wake wa Twitter.


“Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli, amempigia simu na kumpa pole Mhe. Zitto Zuberi Kabwe, aliyepata ajali ya gari jana mkoani Kigoma, amemuombea heri ili apone haraka na pia amewashukuru madaktari na wauguzi wa kituo cha afya cha Kalya na Hospitali ya Maweni kwa matibabu waliyompa”, ameandika Msigwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments