BASHIRU AWAOMBA WATANZANIA KUTOFANYA MAJARIBIO YA UONGOZI

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally, amewaomba watanzania kutofanya majaribio ya uongozi wa nchi kama baadhi ya vyama vinavyoendelea kuwalaghai kwa kuomba kujaribiwa.

Ameyasema hayo tarehe 10 Oktoba, 2020 katika mkutano wa kampeni jimbo la Ukonga.

“Hakuna Chama kingine mpaka leo tunapozungumza chenye uzoefu na uwezo wa kulinda umoja, upendo na mshikamano wa Taifa hili isipokuwa CCM.”

“Ndugu zangu, ninawaomba tusiwajaribu watu wasio na uzoefu, CCM inaouzoefu, inaweza kuwa na upungufu fulani kwa kuwa ni Chama cha watu sio cha malaika, lakini katika eneo la kulinda uhuru, Usalama, amani, umoja, mshikamano wa kitaifa na muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Hakuna Chama kingine cha kukupa uhakika katika hayo isipokuwa CCM.”


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments