Tanzia : ALIYEKUWA KAMANDA WA POLISI ARUSHA JONATHAN SHANA AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa Kamanda wa Polisi mkoani Arusha Jonathan Shana amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.


Taarifa ya kifo chake imethibitishwa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Hospitali ya Taifa Muhimbili Aminiel Aligaesha na kusema kuwa marehemu alikaa hospitali kwa siku 21 na kati ya hizo alikaa katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), kwa siku tatu.

Kamanda Shana aliwahi kuwa Kamanda wa Polisi (RPC) katika Mkoa ya Pwani, Mwanza na Arusha.

ACP Jonathan Shana amefariki akiwa Afisa Mnadhimu Namba Moja katika Chuo cha Polisi (CCP) mkoani Moshi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527