MLIPUKO MKUBWA WATOKEA MJI MKUU WA LEBANON, BEIRUT NA KUSABABISHA MADHARA MAKUBWA


Mlipuko mkubwa umetokea katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut.Mlipuko huo umeiharibu kabisa sehemu kubwa ya bandari na majengo katika maeneo mbalimbali ya mji huo.

Maafisa wamesema zaidi ya watu 60 wamefariki na wengine zaidi ya 3,000 wamejeruhiwa, huku miili ikiwa imefukiwa katika vifusi.

Saa chache baadaye, magari ya kubebea wagonjwa yalikuwa yakiwabeba majeruhi huku helikopta za jeshi zikisaidia kuuzima moto mkubwa uliokuwa ukiendelea kuwaka katika bandari hiyo.

Chanzo cha mlipuko huo, uliosababisha moto mkubwa, kupindua magari madogo na kuvunja madirisha na milango, hakikujulikana mara moja.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527