MACHO, MASIKIO YAELEKEZWA DODOMA UTEUZI WA WAGOMBEA URAIS WA TANZANIA KATIKA UCHAGUZI MKUU 2020

Macho na masikio ya Watanzania wengine yanaelekezwa Jiji la Dodoma kutakakofanyika uteuzi wa wagombea urais wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.


Uteuzi huo unafanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) katika ofisi zake zilizopo Ndejembi nje kidogo ya Jiji la Dodoma. 

Pia, leo hiyohiyo kutafanyika uteuzi wa wagombea ubunge na udiwani nchini nzima.

Uteuzi wa urais, hii ni mara ya kwanza, NEC kuendesha shughuli hiyo Dodoma baada ya kuhamia huko ikitokea jijini Dar es Salaam.

Joto la wagombea 17 waliochukua fomu zinapanda na kushuka wakisubiri kuona Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) itamteua nani na kumwacha nani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527