Breaking : RAIS MAGUFULI AMEFANYA UTEUZI MWINGINE USIKU HUU LEO ALHAMIS



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Julai 9,2020 amefanya uteuzi wa Mkuu wa wilaya mmoja na Mkurugenzi Mtendaji mmoja kama ifuatavyo.


Rais Magufuli amemteua Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Advera Bulimba kuwa mkuu wa wilaya ya Nzega mkoani Tabora huku akimteua Solomon Isack Shati kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Hanang mkoani Manyara.


Wakati huo huo, Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Kept, (Mst) George Huruma Mkuchika kwa mamlaka aliyokasimiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa wilaya 2 kama ifuatavyo.


Mkuchika amemteua Omary Mwanga kuwa katibu tawala wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi huku akimteua Saitot Zelothe Stephen kuwa katibu tawala wilaya ya Mbeya mkoani Mbeya.




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527