TAKUKURU KAHAMA YAOKOA SHILINGI MILIONI KUMI NA TANO ZA WALIMU WASTAAFU NA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NGAYA



Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mh. Anamringi Macha (kulia) akikabidhi fedha zilizookolewa kwa mmoja  waWalimu wastaafu, katikati ni Mkuu wa TAKUKURU Wilaya ya Kahama ndg. Cosmas Shauri

TAARIFA KWA UMMA.

TAKUKURU KAHAMA YAOKOA SHILINGI MILIONI KUMI NA TANO ZA WALIMU WASTAAFU NA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NGAYA
HALMASHAURI YA WILAYA YA MSALALA.

Ofisi ya TAKUKURU mkoa wa Shinyanga inaendelea na uchunguzi wa ubadhirifu wa fedha katika Chama cha Akiba na Mikopo cha Walimu Kahama (WALIMU KAHAMA SACCOS LTD). Fedha hizi kiasi cha Sh. 7,780,625/= zilizookolewa zitalipwa moja kwa moja kwa Walimu Wastaafu wanaokidai Chama Cha Akiba na Mikopo cha Walimu Kahama (WALIMU KAHAMA SACCOS LTD) na Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Mhe. Anamringi Macha.


Aidha katika uchunguzi uliofanyika kuhusiana na ujenzi wa Kituo cha Afya cha NGAYA kilichopo kata ya NGAYA Halmashauri ya Msalala, Ofisi ya TAKUKURU (W) Kahama imefanikiwa kuokoa kiasi cha shilingi 7,275,500/= ambazo zitakabidhiwa leo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama  Mhe. Anamringi Macha kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya MSALALA Ndugu. Simon Berege.

Kwa hiyo jumla ya fedha zilizookolewa na ambazo zitalipwa kwa walimu wastaafu na kukabidhiwa Halmashauri (W) Msalala ni sh. 15,056,125.00.

      DENI LA WALIMU WASTAAFU.
Uchunguzi uliofanyika na TAKUKURU mkoa wa Shinyanga kwa WALIMU KAHAMA SACCOS LTD umebaini kwamba chama hiki kinadaiwa na walimu wastaafu ishirini na tisa (29) jumla ya sh. 13,396,425.00. Deni hili linatokana na akiba za walimu wastaafu walizokuwa wanachangia wakati wakiwa kazini baada ya kustaafu akiba hizi hazikuweza kupatikana kwa kuwa chama kilikuwa hakina fedha.

Barua zote zitumwe kwa Mkuu wa TAKUKURU Mkoa, Mtaa wa Uzunguni, S.L.P. 37, 37101SHINYANGA. Unaweza pia kuwasiliana nasi kwa njia ya simu ya Bure 113, instagram: takukuru.tz, Facebook:  TakukuruTz, Twitter:  TAKUKURU.TZ, Online TV:  TAKUKURUTV



Awamu ya kwanza ofisi ya TAKUKURU (W) Kahama iliokoa jumla ya sh. 5,815,800.00, fedha hizi zililipwa kwa walimu wastaafu kumi na tatu (13) waliokuwa wanakidai Chama cha Akiba na Mikopo cha Walimu Kahama SACCOS.

Katika awamu hii ya pili Ofisi ya TAKUKURU (W) Kahama imefanikiwa kuokoa kiasi cha sh. 7,780,625.00 fedha ambazo zitalipwa kwa walimu wastaafu kumi na sita (16) waliosalia ambao walikuwa wnanchama wa WALIMU KAHAMA SACCOS LTD.

FEDHA ZA UJENZI WA KITUO CHA AFYA NGAYA ZILIZOOKOLEWA SH. 7,275,500/=

TAKUKURU Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ilifanya uchunguzi kuhusiana na ujenzi wa Kituo cha Afya cha NGAYA kilichoko kata ya NGAYA Halmashauri ya Msalala ambapo katika uchunguzi huo ilibainika kuwa kiasi cha sh. 7,275,500/= kimepotea kutokana na Mtaalamu kitengo cha manunuzi kutotekeleza majukumu yake ipasavyo; hivyo ofisi ya TAKUKURU Wilaya ya Kahama kwa kushirikiana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Msalala, imefanikiwa kuokoa fedha hizo. Kwa kuwa kuna kazi ambazo hazijakamilika za ujenzi wa zahanati hiyo, fedha hizo zitakabidhiwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Msalala.

WITO.
TAKUKURU (M) SHINYANGA inatoa wito kwa watumishi wa umma mkoani humu kufanya kazi kwa weledi, uadilifu, uzalendo, uaminifu na kwa kufuata sheria zote za nchi ili fedha zinazotolewa na Serikali kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbali mbali zitumike kama ilivyokusudiwa. Iwapo mtumishi wa umma (mtaalam) atashindwa kuwajibika ipasavyo na hivyo kusababisha upotevu wa fedha ya Serikali mtumishi huyo atarejesha fedha iliyopotea na hatua nyingine za kisheria zitafuata ikiwemo ya kumfikisha mahakamani.

Aidha TAKUKURU mkoa wa Shinyanga inatoa wito kwa Watumishi wa Umama mkoani humu kufichua vitendo vya rushwa vinavyotokea katika maeneo yao ya kazi. Wapo watumishi wananwake ambao wanaombwa rushwa ya ngono ili waweze kupatiwa upendeleo mfano kupandishwa cheo, kupatiwa uhamisho, kupatiwa ruhusa ya kwenda masomoni na huduma nyingine zinazofanana na hizo. TAKUKURU (M) SHINYANGA inatoa wito kwa watumishi wanaokutana na vitendo hivi kutoa taarifa ili wahusika wachukuliwe hatua mara moja.


Imetolewa leo tarehe 02/07/2020 na Mkuu wa TAKUKURU (W) Kahama Kwa Niaba ya Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Shinyanga.

Barua zote zitumwe kwa Mkuu wa TAKUKURU Mkoa, Mtaa wa Uzunguni, S.L.P. 37, 37101SHINYANGA. Unaweza pia kuwasiliana nasi kwa njia ya simu ya Bure 113, instagram: takukuru.tz, Facebook:  TakukuruTz, Twitter:  TAKUKURU.TZ, Online TV:  TAKUKURUTV


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527