MWENYEKITI WA CHAMA CHA WANANCHI (CUF), PROFESA IBRAHIM LIPUMBA AMSIMAMISHA NAIBU KATIBU MKUU ZANZIBAR


Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba  amemsimamisha Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zanzibar, Faki Suleiman Khatib kwa alichokidai ni kuimarisha kamati tendaji ya chama hicho.

Taarifa ya CUF kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo Julai 4,2020 imesema hatua hiyo ni katika kutekeleza agizo la Baraza Kuu la kuondoa Mapungufu na Kuimarisha Kamati Tendaji.

Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu Zanzibar itajazwa na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa linalotarajiwa kuketi mwishoni mwa mwezi huu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527