MSANII wa muziki wa Bongo Fleva nchini Hamisi Mwinjuma alimaarufu Mwana FA amesema kifo cha aliyekuwa Rais wa awamu ya tatu Benjamini Mkapa kimemuumiza na ni pigo kubwa kwa wasanii kutokana na mchango wake wa kuanzisha Cosota.
Mwana FA aliyasema hayo leo wakati akizungumza katika wa ibada maalumu ya maombolezo iliyofanyika wilayani Muheza kwenye viwanja wa Jitegemee na kuongozwa na Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo na wananchi wakiwemo viongozi wa dini. Alisema kutokana na msiba huo mzito ndio maana akaamua kuungana na wananchi wa wilaya ya Muheza katika halfa hiyo kwa sababu katika kipindi chake ndio miongoni mwa taasisi aliyonzisha katika kusimamia haki za wasanii.
Msanii huyo alisema Cosota ni taasisi inayoshughuli na haki miliki za wasanii tokea ilipoanzishwa 1996 na imekuwa na mchango mkubwa kwani kabla ya hapo kazi za wasanii zilikuwa huwezi kumpeleeka mtu mahakamani. Hata hivyo alisema kutokana na hilo wana mshukuru Hayati Mkapa kutokana na mambo makubwa aliyowafanyia wasanii hapa nchini ambayo yamekuwa na tija kubwa kwao .
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin