FREEMAN MBOWE APITA KURA ZA MAONI UBUNGE HAI


Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Upinzani Tanzania Chadema Freeman Mbowe ameshinda kura za maoni za kuwani Ubunge wa Hai Mkoa wa Kilimanjaro katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe 28 Oktoba 2020.

Mbowe amepigiwa kura za maoni jana Jumamosi tarehe 25 Julai 2020 na wajumbe wa mkutano mkuu wa Jimbo hilo uliofanyika ukumbi wa KKKT jimboni humo akiwa mgombea pekee wa nafasi hiyo.

 Akitangaza matokeo hayo, msimamizi wa uchaguzi huo, Michael Kilawaila amesema, Mbowe alipigiwa kura 203 za ndio na mbili za hapana.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527