MTANGAZAJI MAARUFU WA CLOUDS FM HAMISI MANDI 'B DOZEN' ATIMKIA E-FM


Aliyekuwa mtangazaji wa kituo cha Redio cha Clouds FM Hamis Mandi maarufu B Dozen amejiunga na Kituo cha redio cha EFM- Tanzania.


Mandi ambaye anafahamika zaidi kwa jina la utangazaji la B-Dozen (The Navigator, Msafiri) kwa muda mrefu alikuwa akiongoza kipindi cha XXL cha Clouds FM, pamoja na vingine.

Kupitia ukurasa wao wa Instagram, E-FM wameandika mbobezi huyo wa utangazaji amejiunga nao, na kwamba kinachofuata ni kupaa juu, na kuhakikisha mafanikio zaidi kwa Tanzania.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527