KAMPUNI YA FINTECH YAZINDUA APP ITAKAYOSAIDIA KUTOA USHAURI KATIKA MASUALA YA KIFEDHA

Kampuni ya Fintech imezindua App mpya ambayo itakayokuwa ikitoa ushauri wa kifedha kwa mtu binafsi kulingana na mapato na matumizi yake, kutumia akili bandia (Artificial Intelligence) ambayo ni teknolojia ya hali ya juu.

App ya Mipango, inayojihusisha na masuala ya kifedha, itasaidia Watanzania kuwa na uelewa mzuri juu ya matumizi yao, mapato yao na kupata nafasi ya kuangalia bajeti binafsi, kujiwekea malengo ya maendeleo na kisha app hii kukusimamia ili kufanikisha malengo hayo. Ikiwalenga watanzania wa rika zote na kisomo chochote, Mipango app inapatikana kwa lugha ya Kiswahili huku elimu ya fedha ilikitolewa kwa lugha rahisi Zaidi. 

Kwa mujibu wa mmoja wa Waanzilishi wa Mipango, Bi. Lilian Makoi: “Kua na elimu ya kifedha ni moja ya nguzo ya kukua na maendeleo nchini. Zaidi ya  asilimia hamsini (50%) ya  watu wazima wa Watanzania hawajui kiasi au jinisi wametumia  fedha zao wiki iliyopita, na hawana malengo ya kifedha. Tabia hiyo inaingiza watu kwenye madeni mabaya, ambayo inaongoza kupelekea kuwa masikini.”

“Tumeamua kuzindua App hii kwa lengo la kutoa fursa ya kubadilisha maisha ya raia wetu wanayoishi kila siku na kuwa na mahusiano mazuri na fedha zao. Program hii itamsadia mteja kupokea ushauri wa kifedha bure, kufuatilia kipato chake, kufuatilia matumizi yake yote yanavyokwenda, kusimamia mikopo na madeni na pia kupata fursa za uwekezaji kuendana na kipato chake,” alisema Lilian. 

Aliongeza: “Pia tunatarajia kupata zaidi ya watu milioni moja ambao watapakua  App hii ndani ya miezi 12 ya mwanzo.  Mwaka 2017 taasisi ya Finacial Sector Deepeing (FSDT), walifanya utafiti wa sekta ya fedha katika miji mbalimbali na kujua kuna watu zaidi ya milioni 27 walikuwa watumiaji hai wa simu Tanzania na 48.7% kati ya hao ni watuamiji wa simu za mkononi zenye kuweshwa huduma za mtandao (Smart Phones). Kati ya watumiaji hawa wa simu, milioni 9 ndio wenye vyanzo vya mapato. Hii ilitupelekea kuamini kwamba kuzindua App hii itakuwa na manufaa zaidi kwa raia wa nchi hii.”

Katika miji mingine kwa kipindi cha miezi 12 iliyopita, asilimia 43 ya Watanzania walitunza fedha zao nyumbani kwa njia ya mtandao au kwa benki au kwa watu wa karibu wa familia.

Mwanzilishi mwingine wa Mipango Fintech, Agness Mollel alisisitiza: “Fikra zetu kwa baadaye ni kuwashawishi vijana wengi Zaidi kua na Mipango binafsi ya kifedha na kuwawezehsa kufikia malengo yao kwa kutumia fursa za kuwekeza zinazowafaa nchini. 

Lengo letu ni kuwa wezesha watu katika maeneo yote na wenye umri tofauti kkua na Mipango ya kifedha na matumizi mazuri kwa mafanikio yao binafsi,”.

“App hii itakuwa ikitambulisha kitu kipya kila mwezi, ikiwa ni pamoja na kuwawezesha wateja wetu kununua hisa na fursa za uwekezaji, kutunza kumbukumbu za ulio wakopesha na kupata ushauri wa kila matumizi unayoyafanya kulingana na uwezo wako halisi wa kifedha.” Ofisa Mkuu wa Teknolojia wa kampuni hiyo, Nicholaus Ngolongolo, alisisitiza. 

“Uzinduzi huu una vipengele vitatu ambavyo ni kutengeneza wasifu wako wa kifedha, kutengeneza bajeti ya mwezi na kurekodi mapato na gharama za kila mwezi/ siku ambazo zitakuwa zikifuatiliwa kulingana na bajeti yako ili kukusaidia kuishi ndani ya bajeti yako!” alimalizia Mwanzilishi wa nne Chris Rabi.

Uvumbuzi mpya wa huduma hii kwenye simu za mkononi unaletwa na Kampuni ya Mipango Fintech ambayo itabadilisha Watanzania jinsi ya kuishi kwa malengo na usimamizi wa fedha zao binafsi na kuwezesha kufikia malengo yao ya maendeleo.  Hii ni hatua ya kwanza ila tunategemea kuendelea kutambulisha vipengele vingine vingi Zaidi na Zaidi.

Kuhusu Mipango Fintech 
Mipango ni huduma binafsi ya fedha ambayo inamwezesha mtumiaji kutunza fedha, matumizi, malengo ya fedha, bajeti na kuwekeza kupitia fursa za kifedha. Mtumiaji wa Mipango app anaweza kupata uelewa zaidi juu ya kuzimiliki fedha zake kwa uhuru zaidi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527