CHINA NAYO YAGEUKIA MITISHAMBA KUTIBU CORONA


Wakati wanasayansi wakipambana kutengeneza chanjo ya virusi vya corona, China nayo imetengeneza dawa ya asili inayojulikana kama 'Traditional Chinese medicine (TCM)' ili kutibu ugonjwa wa corona.


Gazeti moja lililozinduliwa na serikali ya China lilidai kuwa 92% ya wagonjwa wa corona wa nchi hiyo walitibiwa na dawa hiyo. TCM ni dawa ya kale zaidi duniani ambayo imetengenezwa kwa mitishamba.

Dawa hiyo ni maarufu sana nchini China licha ya kwamba ilizua mjadala kuhusu matumizi yake mtandaoni.

Wataalamu wanasema China inajaribu kuisambaza dawa hiyo ya TCM ndani ya nchi na nje ya nchi lakini wataalamu wa afya bado hawaamini uwezo wake wa kutibu.

Wizara ya afya ya China imeweka kitengo maalum cha TCM pamoja na muongozo wa kukabiliana na virusi vya corona, wakati televisheni ya taifa ilidai kuwadawa hiyo ilifanya kazi katika mlipuko wa miaka ya nyuma kama Sars mwaka 2003.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527