WHO YASITISHA MAJARIBIO YA HYDROXYCHLOQUINE KAMA TIBA YA CORONA


Shirika la Afya ulimwenguni WHO, limesema linaahirisha majaribio ya dawa ya hydroxychloroquine kama tiba ya ugonjwa wa COVID-19. 


Mkuu wa shirika hilo Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema wanachunguza usalama wa dawa hiyo.

Uamuzi huo wa WHO umefikiwa baada ya ripoti ya wanasayansi iliyochapishwa katika jarida maarufu la kitabibu la The Lancet wiki iliyopita, ikisema matumizi wa hydroxychloroquine yalikuwa yakizidisha hatari ya kufa miongoni mwa wagonjwa wa COVID-19, amesema mkuu wa shirika hilo Tedros Adhanom Ghebreyesus katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwa njia ya video jana jioni.

Tedros alisema kile kinachofahamika kama 'mshikamano wa majaribio' kinachohusisha mamia ya hospitali ulimwenguni ambazo zimekuwa zikiijaribu dawa hiyo kwa wagonjwa wa virusi vya corona kimeacha majaribio hayo kama hatua ya tahadhari tu. Mkuu wa huduma za dharura katika shirika la WHO Mike Ryan amesisitiza kuwa hakuna matatizo mengine yaliyojitokeza.

Ingawa dawa hiyo awali ilitumiwa kutibu malaumivu ya misuli, baadhi ya watu, rais Donald Trump wa Marekani miongoni mwao, wamekuwa wakiipigia debe kama tiba kwa virusi vya corona, na nchi kadhaa zimekuwa zikiiagiza kwa wingi. Wiki iliyopita, waziri wa afya wa Brazil alishauri matumizi ya dawa hiyo, pamoja na nyingine ya Chloroquine inayotibu malaria, kwa ajili ya wagonjwa wa COVID-19.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527