WAGONJWA WA CORONA NCHINI KENYA WAFIKA 758 BAADA YA WENGINE 21 KUONGEZEKA

Wizara ya afya  nchini Kenya imesema  kuwa maambukizi ya virusi vya Corona nchini Kenya yamefikia 758 baada ya watu 21 zaidi kuthibitishwa kuwa na virusi vya Corona baada ya sampuli 1486 kupimwa katika muda wa saa 24 zilizopita.

Aidha idadi ya waliofariki imeongezeka na kufikia 42 baada ya watu wawili zaidi kufariki hapa Nairobi.

Vilevile idadi ya waliopona imefikia 284 baada ya watu wengine 3 kupona na kuondoka hospitalini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527