WAGONJWA WA CORONA NCHINI KENYA WAFIKA 715


Watu waliofariki kutokana na Virusi vya Corona nchini Kenya wamefikia 36, Walioambukizwa 715 huku watu 259 wakiwa wamepona na kuruhusiwa kurudi nyumbani.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya nchini humo imeeleza kuwa Mtoto wa mwaka mmoja na miezi minane ni miongoni mwa waliotambuliwa kuwa na virusi hivyo baada ya sampuli 978 kufanyiwa vipimo katika saa 24 zilizopita.

Naibu Waziri wa Afya Dkt.Rashid Aman ameeleza kuwa raia wawili wa Tanzania ni miongoni mwa waliothibitishwa kuwa na virusi vya Corona katika kituo cha mpakani cha Isebania baada ya kupimwa na hivyo wamerejeshwa Tanzania.

Aidha wizara hiyo ya Afya imefafanua kuwa watu wawili walifariki wakiwa nyumbani na mwingine mmoja akiwa hospitalini ambao wamefikisha idadi ya waliofariki kufikia 36, huku maambukizi mapya 15 ya virusi vya Corona yaliyofanya idadi 715 ya walioambukizwa


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527